JOHARI AGOMA KUKATA MAUNO YAKE MBELE YA RAY
Posted by Bigie habari za kitaifa, JOHARI 12:03 AMMKONGWE kwenye ‘Industry’ ya Filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ alitoa kali ya aina yake baada ya kukataa kuzungusha nyonga mbele ya mwigizaji mwenzake, Vincent Kigos ‘Ray’ anayedaiwa ni mpenzi wake
Tukio hilo lililonaswa na mwandishi wetu juzikati, lilitokea katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar wakati wasanii hao walipojumuika pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kitokee kifo cha msanii mwenzao, Steven Kanumba.
Akiwa viwanjani hapo, Johari aliitwa kupanda jukwaani na wasanii wenzake kwa ajili ya kucheza sebene kidogo lakini yeye alikataa na mwandishi wetu alimsikia akijitetea kuwa hawezi kukata nyonga mbele ya wasanii wenzake hususan Ray ambaye ni bosi mwenzake kwenye kampuni yao ya RJ Company.
“Siwezi kujidhalilisha mbele ya umati huo kwa kukata kiuno tena na bosi mwenzangu yupo pale, labda ningekuwa nimelewa kiasi cha kutojitambua hapo ningefanya madudu kama hayo,” alisema Johari.
GPL
"RAY HAYAJUI MAUMBILE YANGU NA SINA UHUSIANO NAYE".....JOHARI
Posted by Bigie BONGO MOVIE, habari za kitaifa, JOHARI 11:41 PMMSANII wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amefunguka kuwa, licha ya watu kudai kuwa yeye ana uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzake Vincent Kigosi ‘Ray’, anaapa hawajawahi kufikia hatua hiyo.
“Naapa sijawahi kulala na Ray. Nashangaa hizi habari zinavyozidi kuenea. Kwa hilo niko tayari kushika hata Biblia kuapia kuwa sina na wala sijawahi kuwa na uhusiano na Ray, uhusiano wetu ni wa kikazi tu,” alisema Johari.
Johari kwa muda mrefu amekuwa akidaiwa kutoka na Ray kwa siri lakini mwenyewe anakana huku wadau wakizidi kushikilia kuwa habari hizo zina ukweli ndani yake.
"MBWA WANGU HUNIONDOLEA MAWAZO NA KUNIFARIJI"....JOHARI
Posted by Bigie BONGO MOVIE, habari za kitaifa, JOHARI 12:09 AMSTAA wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema kuwa anapokuwa nyumbani kwao marafiki zake wakubwa ni mbwa wake wawili ambao anawafuga kwa sasa.
Akiongea kwa kujiamini, Johari alisema kuwa mbwa hao huwa wanamsaidia pindi anapokuwa na mawazo kwani humchangamsha pale anapocheza nao.
“Unajua nawapenda sana mbwa wangu na sijui ni kwa nini nilichelewa sana kuwatafuta, mara nyingi hunifariji wakati ninapokuwa na mawazo mabaya,” alisema Johari.
Mbali na mbwa hao, pia Johari alisema kuwa siku mojamoja huenda kuchungulia katika bendi mbalimbali za burudani kwa ajili ya kuchangamsha akili yake.A
.
Featured Post
NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne ambayo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...



