AGNESS GERALD "MASOGANGE" ACHUMBIWA


MREMBO  anayeuza nyago katika video za wanamuziki wa Bongo Fleva na muvi za Kibongo, Agness Gerald ‘Masogange’, amechumbiwa nje ya Tanzania.

Akizungumza na mpekuzi wetu   juzikati, Agness aliweka kweupe kuwa, amevishwa pete ya uchumba na mwanaume anayemtosheleza kwa kila kitu ambaye siyo Mbongo  na kifuatacho ni ndoa itakayofungwa muda si mrefu.

Alifunguka: “Ndoa itafungwa nchini kwa huyo mwanaume, lakini taratibu nyingine zote kama send-off zitafanyika hapa Bongo.”

Agness aliweka wazi kuwa  hakuwa tayari kuolewa Bongo kwa sababu wanaume wengi ni wazinguaji na hawana mapenzi ya dhati.

Mrembo huyo mwenye umbo tata alisema kuwa pamoja na kuwaambia amechumbiwa, wanaume wameendelea kumtokea kila kukicha.

Posted by Bigie on 4:47 AM. Filed under , , , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.